Jumapili. 05 Mei. 2024

Mt. Benedicto , Abate

Benedicto , Abate

Mama Kanisa anatuomba tuungane naye katika sherehe kwa heshima ya Mtakatifu Benedict aliyezaliwa March 2, 480 huko Nursia, Umbria katika ardhi ya Taifa la Italia. Alipelekwa Roma kusoma lakini hakuridhishwa na mazingira ya pale.

Mwaka 500 Mtakatifu Benedict aliamua kuacha masomo yake na akaamua kwenda Subiaco, akakaa huko peke yake pangoni akisali.

Baadaye akaombwa na Jumuia ya Watawa waliokuwa wakiishi katika Monasteri ya Vicovaro kuwa Abate wao.

Mtakatifu Benedict aliweka sheria ngumu na kufuata kikamilifu maisha ya kitawa na baada ya muda yakafanyika majaribio kadhaa ya kumuua.

Mtakatifu Benedict akaondoka hapo na kwenda kuishi tena pangoni peke yake na huko napo akakutana na watu waliotaka kumletea matatizo na hivyo akaondoka tena mwaka 530.

Kutokea hapo Mtakatifu Benedict alizunguka sehemu mbalimbali na kuanzisha monasteri 12 na mwisho akaanzisha Monasteri ya Monte Cassino iliyokuwepo kati ya Roma na Naples.

Mtakatifu Benedict alikufa mwaka 547 huko Monte Cassino na Baba Mtakatifu Humorous III akamtangaza Mtakatifu mnamo mwaka 1220 .

Maoni


Ingia utoe maoni