Jumapili. 19 Mei. 2024

Mt. Wenyeheri Yakobo wa Sale na William, Wafiadini

Wenyeheri Yakobo wa Sale na William, Wafiadini

Yakobo wa Sale alizaliwa Ufaransa mwaka 1556. Baba yake alikuwa Mtumishi wa Askofu. Yakobo aliingia shule ya Majesuiti akapewa Upadre.

William alikuwa mtumishi katika shule ile ile na baadaye aliingia shirika la Majesuiti akawa Bruda.

Wote wawili walikwenda kuhubiri katika Ufaransa na wakati huo Waprotestanti walikuwa wakali sana na waliwaua Wakatoliki. Usiku mmoja Majesuiti hao walishikwa na Waprotestanti, na Padre Yakobo alipigwa Bunduki wa kwanza, na baadaye umati wa watu wakawageukia wale wawili na kuwaua. Hii ilifanyika tarehe 7 Februari 1593. Walitangazwa kuwa Wafiadini Wenyeheri mwaka 1926.

Maoni


Ingia utoe maoni