Jumapili. 08 Septemba. 2024

Tafakari

Alhamisi, Septemba 29, 2016

Alhamisi, Septemba 29, 2016.
Juma la 26 la Mwaka


Sikukuu ya Watakatifu Malaika Wakuu, MIKAEL, GABRIELI NA RAFAELI

Dan 7: 9-10, 13-14 au Ufu 12: 7-12
Zab 137: 1-5
Yn 1: 47-51


JESHI LA MBINGUNI!

Leo tuna adhimisha sikukuu ya Malaika wakuu watatu ambao majina yao yanatajwa katika maandiko: Mikaeli, Gabriel na Rafaeli. Hawa malaika wanaitwa “Malaika Wakuu” maana yake ni wakuu kwasababu wana utume maalumu waliopewa na Mungu. Sikukuu hii ya malaika inatukumbusha kwamba vitu vinavyo onekana na kushikika ni sehemu ndogo sana ya ukweli halisi na hatuwezi kujifanya kujua kila kitu. Siku hizi tunaweza tusitembelewe na malaika kama alivyomtembelea Bikira Maria wakati wakutangazwa kuzaliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo au kipindi cha kutangaza ufufuko wa Yesu, lakini Mungu anaendelea kuwasiliana nasi kwa namna ya pekee. Swali ni kwamba, mimi nipo wazi kiasi ghani Mungu anapotaka kuongea nami?

Sala: Baba wa Mbinguni, umetupa malaika wakuu ili kutusaidia sisi wahujaji hapa duniani. Mtakatifu Malaika Mikaeli ni kinga yetu, namuomba aje kunisaidia, awapiganie wapendwa wangu wote, na atukinge na hatari. Mtakatifu Malaika Gabrieli ni mjumbe wa habari njema, namuomba anisaidie kusikia sauti yako na anifundishe ukweli. Mtakatifu Malaika Rafaeli ni malaika anaye ponya, ninamuomba anipe uponyaji wa yale yote ninayohitaji kuponywa na ya kila mmoja ninaye mfahamu, nyanyua juu katika kiti chako cha neema na utupe tena zawadi yako ya kupona na kuwa huru. Tusaidie Bwana tuweze kutambua kwa ukamilifu kabisa, ukweli wa Malaika Wakuu na hamu yao yakutaka kututumikia. Malaika Watakatifu, Mtuombee. Amina.

Maoni


Ingia utoe maoni