Alhamisi. 19 Septemba. 2024

Tafakari

Jumatano, Agosti 31, 2016

Jumatano, Agosti 31, 2016,
Juma la 22 la Mwaka wa Kanisa

1 Kor 3: 1-9
Zab 32: 12-15, 20-21
Lk 4: 38-44

NGUVU YA MAMLAKA!

Katika Injili ya leo, tunaona Yesu akimponya mkwewe Simoni. Mara nyingi Yesu aliponya kwa kugusa bali pia alikuwa na neno la mamlaka la kuponya kwa kuamuru. Msisitizo unaoneshwa kwenye Injili, ugonjwa ndio unao amuriwa, kama Yesu alivyo amuru mawimbi ya bahari ya Galilaya kwa mamlaka, “hali ikawa shwari” na Amani ikawapo (Mk 4: 39), na mawimbi yakatulia. Je, hili linawezekana kwa mfuasi wa Yesu katika nyakati hizi!. Ukweli ni kwamba amri ya kuamuru inatoka katika mamlaka sio katika nguvu. Kwahiyo tunapaswa kuwa wafuasi tuliojazwa na mamlaka sio nguvu. Hili linawezekana tu, namaanisha tu kwa kukutana na Yesu nakumvaa yeye sio kwakuwa na elimu ya Yesu tu. Ni katika kufikia kiwango cha kusema kama Paulo kuishi kwangu sio mimi bali Kristo anaishi ndani yangu. Twaweza kufanya yote kama tutaunganika na Yesu kweli kweli, si katika kuwa na elimu kuhusu maandiko na kushindwa kuyaruhusu yakufanye uunganike na Yesu. Kwa njia nyingine tumvae Kristo.

Kama tunavyosikia katika somo la kwanza, tumruhusu Mungu akuze maisha yetu, tumuache Kristo afanye mabadiliko ndani yetu. Sisi ni shamba la Mungu tumruhusu Mungu akuze zawadi mbali mbali mioyoni mwetu ili tuweze kuzaa matunda yenye kumpendeza. Tushirikiane na Mungu ili zawadi anazo kuza ndani yetu ziweze kumrudishia sifa na utukufu.

Sala: Bwana, tufanye washiriki wa mamlaka yako. Amina

Maoni


Ingia utoe maoni