Alhamisi. 19 Septemba. 2024

Tafakari

Jumanne, Agosti 30, 2016

Jumanne, Agosti 30, 2016.
Juma la 22 la Mwaka

1 Kor 2: 10-16
Zab 144: 8-14
Lk 4: 31-37


VITA VYA KIROHO!

Leo katika somo la kwanza, Mt. Paulo anaongelea kuhusu Roho wa Mungu na roho wa ulimwengu, vita vya kila wakati katika mioyo yetu, tukivutwa huku na huku. Injili inamuonesha Yesu akitoa pepo, akiamuru “pepo mchafu” atoke ndani ya mtu. Watu wa Kapernaumu huenda walijua mtu yule alikuwa na pepo mchafu, lakini hawakujua nini, au nani, huyo pepo. Hawakuweza kulitambua kwa jina au kufahamu. Lakini Yesu aliweza. Umoja wake na Baba unampa utambuzi ambao wengine hawana. Mt. Inyasi wa Loyola anatumia neno la “utambuzi wa roho” kwa mpangilio uliojikita kwenye Imani kwa nia ya kutambua na kuelewa, nini kinaendelea ndani ya mioyo yetu na nini mapenzi ya Mungu kwa ajili yetu. Tuombe neema ya kutambua machafuko ndani ya mioyo yetu na kuisikiliza sauti ya Mungu.

Sala: Baba Mungu, ninakuomba wewe “Roho ya utambuzi” ili niweze kukua daima na kusikiliza sauti ya Roho wako kwa haraka na kwa ufasaha kila wakati. Amina

Maoni


Ingia utoe maoni