Alhamisi. 19 Septemba. 2024

Tafakari

Ijumaa, Agosti 26, 2016

Ijumaa, Agosti 26, 2016,
Juma la 21 la Mwaka


1Kor 1:17-25;
Zab 32: 1-2, 4-5, 10-11;
Mt 25: 1-13


‘MJINGA’ KWA AJILI YA KRISTO?

“Mungu ndio, Yesu ndio, Kanisa hapana!”. Namna hii ya kufikiri imezoeleka sana kati ya wengi. Je, sisi ni mmoja wao kati ya hawa “wengi”? Je kuna wakati tunajisikia mafundisho ya kanisa ni “yakizamani, yamepitwa na wakati, yasiofikirika na hivyo hayafai kuyaishi”? Na pia hayaendani na zama zetu za sayansi ya hali ya juu? Na hasa kuhusu, maadili na mambo ya maisha ya familia? Je, inawezekana kuwa Wakristo wazuri wanaoenda kanisani kila mara na bado kubaki bila kusumbuliwa na kufuata “majibu ya haraka yanayoonekana” ambayo “wenye hekima na akili” wa ulimwengu huu wanayotoa, wakati mafundisho ya Kanisa yanoonekana kupishana na mambo hayo?

Mafundisho ya Kanisa yanaweza kuonekana kuwa “Msalaba”- lakini hii ni kwasababu hayajajengwa katika “sayansi ya mwanadamu au hekima ya mwanadamu”, bali katika maisha ya Kristo, msulubiwa. Mt. Paulo anatuambia wazi. “ujumbe juu ya Msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu” (1Kor 1: 18). Ni ukuweli usiopingika kwamba, Kanisa linaoongozwa na Roho Mtakatifu, anayetufundisha kila kitu, nakutukumbusha yote aliyofundisha Kristo na kusema kwetu kama alivyotuahidi mwenyewe. (Yn 14: 26). Je, inawezekana kwamba, “wanasayansi na wanafalsafa, watu mashuhuri na wanaojiona wenye akili sana- wanao tetea mawazo yao kwa kutoa hitimisho ya vitu vinavyoonekana –ambavyo kanisa linaona kwamba sio sahihi- kwamba wana akili na hekima zaidi kuliko Mungu aliyewaumba?

“Kwa sababu upumbavu wa Mungu una hekima zaidi ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una hekima zaidi ya wanadamu.”(1 Kor 1: 25). Kufuata anachosema Mama Kanisa huenda kikaonekana upumbavu katika kiwango cha ulimwengu, hii ni kwasababu Mama kanisa anafundisha kuendana na utashi wa Kristo aliyefanya jambo lilionekana kuwa la aibu kwa kufa msalabani ili kutukomboa sisi, wadhambi. Pengine kwako kuungama unaona ni upumbavu au jambo la aibu! Ujue kuungama ni kwaajili ya ukombozi wa roho yako. Sisi tuwe kama Kristo, tukubali kuonekana kuwa wajinga wa ulimwengu huu, kwakufuata mafundisho ya Kristo aliyoyasimika katika Kanisa lake.

Sala: Baba, tupe neema tuwe na utashi kama wa Kristo. Amina

Maoni


Ingia utoe maoni