Alhamisi. 19 Septemba. 2024

Tafakari

Jumanne, Agosti 23, 2016

Jumanne, Agosti 23, 2016,
Juma la 21 la Mwaka

2 Thes 2:1-3, 14-17;
Zab 95:10-13;
Mt 23:23-26


UHURU KWA KUACHANA NA UNAFIKI!

Ipo wazi kutoka katika maisha ya Yesu na mifano kwamba hakulaumu yeyote; alilaumu dhambi yenyewe si mdhambi. Hata leo katika Injili ya leo, analaumu njia ambayo Mafarisayo na Walimu wa sheria, wametumia dini na matendo ya dini vibaya kwaajili ya manufaa ya wao binafsi. Yesu analaumu unafiki wa watu. Katika uhalisia unafiki maana yake ni mtu kujifanya kuwa na kitu ambacho katika hali ya kweli hana. Kusema uongo na unafiki huwa vinaenda sambamba. Yesu hapendi maisha ya namna hii. Katika hali ya maisha ya unafiki maana halisi ya dini inapotea, na hapo dini inakuwa inafanywa kwa njia zisizo eleweka. Yesu aliweza kutambua mara moja waliokuwa waaminifu na wale walikuwa wanafiki. Kwahiyo alilaumu unafiki wao kwa ujasiri kabisa. Wanafiki walijaribu kwa njia zote ili kupata wafuasi. Walipopata mfuasi, maisha yake yanafanywa kuwa maguu kwa kumtambulishia sheria nyingi, mila nyingi za njee na mambo mengi yakufanya. Kwahiyo Watu walipoteza muelekeo kamili wa yaliokuwa ya muhimu katika dini, na kushikilia mambo yasio ya lazima.

Mambo yote, mila na tamaduni za kidini yanapaswa yatuongoze kwa Mungu. Ni njia zinazo tumika katika dini ili kutuleta karibu na Mungu. Ni njia zinazotumika katika dini ili kutuleta karibu zaidi na Mungu, na mambo hayo sio mwisho wa kila kitu, mwisho unapaswa kuwa Mungu. Yesu analaumu aina zote za unafiki zinazomfanya Mungu awe mbali nasi katika matendo yetu ya Imani (dini).

Sala: Mungu Baba yetu wa Mbinguni tuweke huru kutoka katika tabia ya unafiki wetu katika kumfuata Mwanao. Amina.

Maoni


Ingia utoe maoni