Jumatatu. 13 Mei. 2024

Tafakari

Jumanne, Agosti 16, 2016

Jumanne, Agosti 16, 2016,
Juma la 20 la Mwaka
Eze 28:1-10;
Kumb 32:26-28, 30, 35-36;
Mt 19:23- 30


KUACHA YOTE NA KUMFUATA KRISTO!

Kilele cha mwisho kabisa cha mwanadamu ni kujua, kupenda, kumtumikia Mungu na kufurahia maisha ya milele pamoja naye daima. Na Mungu anapenda kutushirikisha uzima huu wa milele. Ni zawadi kutoka kwa Mungu. Hatuwezi kupata uzima huu kwa nguvu za kibinadamu. Tungeachiwa sisi tu, ingekuwa vigumu sana kwetu sisi kuupata. Lakini kwa neema ya Mungu yote yanawezekana. Lakini, mali na utajiri vinaonekana viashiria vinavyo hatarisha kutokuupata ufalme huu wa milele. Katika ulimwengu huu wa sasa wenye mambo mengi inakuwa vigumu kwa wengine kukwepa hili. Ni jambo kubwa la kweli “kuacha yote” lakini kubwa zaidi “kumfuata Yesu”.

Kumfuata Yesu ni kazi yetu. Katika hili linabeba ukombozi wa mwanadamu, lakini hatuwezi kumfuata Kristo kama hatutaacha yote yanayotufunga tushindwe kumfuata. Nabii Ezekiel katika somo la kwanza anatoa angalisho kwa mji wa Tiro na viongozi wake waliopata mafanikio makubwa na nguvu. Wameweka ulinzi wao na Imani yao katika utajiri na mali ambavyo vimegeuka kuwa miungu yao.

Lakini Petro anasema, “tumeacha yote” sio tuu vitu vya ulimwengu, lakini pia tamaa zinazopendwa na mioyo yetu. Wanaobaki wakiwa wameshikilia baadhi ya vitu inakuwa hawajaacha yote. Kwanini anatoa ujumbe mkali namna hiyo kwa matajiri? Kwanini Yesu anaongea sana kuhusu mali? Ni kwasababu mali inaweza kutufanya tusiwe huru au kutupa uhuru wa ouongo. Wengine wameshindwa kumfuata Yesu kwasababu ina maana ya kuacha baadhi ya uhusiano, na wengine kama yule tajiri, ni kwasababu watapoteza nafasi yao ya heshima au njia zao za kupata mali. Wewe je?

Sala: Bwana, naomba nikufanye wewe wa kwanza katika maisha yangu na nikuchague wewe kwa uhuru kamili hata kama kukufuata inagarimu.

Maoni


Ingia utoe maoni