Jumatano. 15 Mei. 2024

Tafakari

Alhamisi, Juni 22, 2017

Alhamisi, Juni 22, 2017.
Juma la 11 la Mwaka

2 Kor 11: 1-11
Ps 111: 1-4, 7-8
Mt 6: 7-15


BABA YETU!

Katika Injili ya leo hatuja alikwa tu kusali bali tunazamiwa kuwa watu wa kusali. Sala ya Bwana ni mwaliko sio tuu wa kusali bali kusali pamoja na wengine. Sala ya Bwana ilitolewa kwetu na Bwana wetu Yesu Kristo, kama njia ya kutufundisha kusali. Lakini, kusema sala hii haitoshi tu. Cha muhimu ni kuzama katika kila kipengele cha sala hii ili iweze kuwa mfano wa maombi yetu kwa Mungu na chombo cha maisha yetu yote kwake.

Sala ya Bwana haijaanza na ombi, bali ina anza na kitambulisho chetu kukubali kwamba sisi ni watoto wa Baba. Huu ni ufunguo wa sala ya Bwana ikisaliwa vizuri. Inafungua pia kila chimbuko la kila sala katika maisha ya Mkristu. Kila Mkristo anapaswa kumuona Mungu kuwa Baba yetu. Tunapaswa kujiona sisi kama watoto wa Mungu ili tuweze kumfuata kama watoto wake. Watoto wana ujasiri kwa wazazi wao bila kujali wanapendwa au la. Hiki kinapaswa kuwa chanzo cha sala zetu zote kila wakati. Tunapaswa kuanza na uelewa kwamba Mungu anatupenda bila kujali hali zetu. Kwa uelewa huu wa Mungu utatusaidia sisi tuwe na ujasiri wa kumuita yeye. Kumuita Mungu “Baba” kunaonesha Agano Jipya lililo anzishwa katika damu ya Yesu Kristu. Neema hii inaonesha pia umoja wetu wa pekee tulio nao katika Yesu Kristo kama Mwana wa Mungu. Kwa hiyo hatuja unganishwa kwa pamoja tu, bali tunawezeshwa pia kumwabudu Yesu kwa pamoja. Umimi huachwa na hivyo kuwa na undugu na umoja. Sisi ni wana wa familia zawadi ya utukufu wa Mungu.

Sala: Babab yetu, uliye Mbinguni jina lako litukuzwe, ufalme wako ufike utakalo lifanyike duniani kama mbinguni, utupe leo mkate wetu wa kila siku, utusamehe makosa yetu, kama tunavyo wasamehe na sisi waliotukosea usitutie katika kishawishi lakini utuopoe maovuni. Yesu nakuamini wewe. Amina.

Maoni


Ingia utoe maoni