Ijumaa. 17 Mei. 2024

Tafakari

Jumatano, Juni 07, 2017

Jumatano, Juni 7, 2017.
Juma la 9 la Mwaka

Tob 3: 1-11, 16-17;
Zab 24: 2-9;
Mk 12: 18-27.


MPE YESU KITI CHA DEREVA WA MAISHA YAKO!

Leo Masadukayo wanataka kumtega Yesu. Lakini jibu la Yesu linakata kiini cha tatizo lenyewe. Anaanza kwa kuonesha kwamba Masadukayo hawayafahamu Maandiko Matakati wala nguvu ya Mungu. Masadukayo walijigamba na aina Fulani ya maisha ambayo iliwafanya wawe na majivuno na hali ya kuji halalisha wao wenyewe kuwa ni wenye haki. Yesu anawaongoza katika hali ya kufikiri vizuri.

Yesu pia leo anatupa changamoto kuhusu uelewewa wetu wa Maandiko Matakatifu na nguvu ya Mungu. Yesu anatusaidia kutambua kuwa mara nyingi tumekuwa na uelewa tofauti kuhusu maisha yajayo. Hisia zetu na hali ya kufikiri kimakosa vinatupeleka kiasi kwamba tunajikuta kwenye njia au mtazamo tofauti usio wa kweli. Wakati tunapojikuta kuwa tumepotea au wakati tunatambua kuwa hatuelewi nguvu ya Mungu ikiwa kazini, tunapaswa kuacha, na kusali kutafuta kile ambacho Mungu anataka kutuambia. Tunapaswa kushuka chini kwa unyenyekevu na kukiri kwa Mungu na nafsi zetu kwamba hatufahamu njia zake na mapenzi yake. Tunapaswa kumsikiliza Mungu achukue nafasi ya kuongoza maisha yetu.

Sala: Bwana, ninatamani kufahamu ukweli. Wakati mwingine najikuta mwenyewe nikijiongoza kwenye njia isio sawa. Nisaidie mimi niweze kujinyenyekesha mwenyewe chini yako ili uweze kuniongoza. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Maoni


Ingia utoe maoni