Jumatatu. 29 Aprili. 2024

Tafakari

Jumatatu, Mei 22, 2017

Jumatatu, Mei 22, 2017.
Juma la 6 la Pasaka

Mdo 16: 11-15;
Zab 149: 1-6, 9;
Yn 15:26 - 16:4.

ROHO MTAKATIFU: MSAIDIZI

Kanisa lenye msingi wake kwa Yesu linaongozwa na Roho Mtakatifu tangu Pentekoste. Mtakatifu Paulo na wengine walihubiri Injili ya Yesu. Sehemu yeyote lilipo hubiriwa neno la Mungu, Roho Mtakatifu ndiye aliyesababisha wongofu wa mioyo ya watu. Lidia alimsikia Paulo na wengine wakihubiri Injili ya Yesu. Alifungua moyo wake kwa Bwana. Ina maana kwamba kwanza kabisa alifungua masikio yake akamsikiliza Yesu, naye Roho Mtakifu akamtia nguvu. Moyo wake na utayari wake wakukaribisha ujumbe wa Kristo moyoni mwake haukuwa tuu kwaajili yake binafsi bali ulibadilisha nyumba yake yote.

Wafuasi walimsikiliza Yesu akiwaambia kwamba watafukuzwa katika masunagogi na hata kuuwawa, maneno haya hawakuyaelewa. Huenda iliwasumbua kidogo, lakini mara moja kwenda kwa mambo mengine ili wasiyawaze zaidi na kuwasumbua. Na bila shaka mitume walipo adhibiwa na Mafarisayo na waandishi, waliyakumbuka maneno haya ya Yesu. Walitambua walipaswa wawaongoze kwenda kwa Mungu, wana sababisha adha katika maisha yao. Watakuwa walijaribiwa katika hali ya kutaka wapoteze Imani yao. Lakini Yesu alitabiri jaribu hili kuu litakuja, lakini akawaonya na kuwaambia kuwa yatakuja.

Lakini kinacho vutia ni kile ambacho Yesu hakusema. Hakuwaambia kwamba watapigana na kurudisha, kuanza fujo, au mapinduzi yeyote nk. lakini tunamuona Yesu akiwaaambia Roho Mtakatifu ndiye atakaye shughulika na hayo. Atawaongoza na kuwawezesha kumshuhudia Yesu. Kuwa mkristo maana yake umekubali mateso.
Roho Mtakatifu anaitwa “Msaidizi”, huwafariji waamini, hasa wakati wauhitaji na mateso. Pia, wakati mwingine kile tunacho dhani ni ukweli kinaweza kisiwe ni ukweli kabisa, kinaweza kuchanganywa na uongo. Yeye pia ni “Roho wa Ukweli”, anayetuonyesha ukweli- kwamba ni Yesu aliyesema ‘mimi ni ukweli, njia na uzima’ (Yn 14:6). Leo tujiulize kama maisha yetu yanaongozwa na Roho Mtakatifu?

Sala: Bwana, ninapo elemewa na mzigo wa ulimwengu au mateso nipe Amani ya mwiili na Roho. Ninaomba unipe nguvu kwa uwezo wa Roho Mtakatifu ili niweze kuwa shahidi wako. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Maoni


Ingia utoe maoni