Jumatatu. 29 Aprili. 2024

Tafakari

Alhamisi, Mei 18, 2017

Juma la 5 Pasaka

Mdo 15: 7-21;
Zab 96: 1-3,10 (K. 3);
Yn 15: 9-11.


KUONGEA LUGHA YA MUNGU!

Wanadamu wanatamani kupendwaa na kujaliwa. Lakini ni vigumu kwa njaa ya upendo kutimizwa, katika hali ya kibinadamu. Leo, Yesu anaongea kuhusu upendo unaozalisha furaha isiyo pimika, ambayo ni Baba na Yeye anayo tu kwa wale walio wake. Hatuwezi kumzidi Mungu kwa mapendo kwasababu anatupenda bila kipimo, kwa upendo unaotoa neema, uzima, Amani na furaha.

Upendo wa Mungu ni kamili na hauwezi kuingiliwa. Upendo wa Baba kwa Mwanae ni kamili katika nyanja zote. Hauna masharti na unakamilisha yote. Ni kamili na hauna ubinafsi. Kwa kupokea upendo wa Baba, Yesu alipokea yote aliyo hitaji. Upendo aliopokea Yesu kutoka kwa Baba yake hauwezi kuondolewa. Hauwezi kuwekwa kwa ubinafsi. Unatiririka kutoka katika moyo wa Yesu na kuja kwetu. Mtiririko huu wa upendo, tuliopewa sisi, hauwezi kufungwa ndani ya mioyo yetu bila kwenda kwa wengine. Hivyo kama tunataka kuwa wapokeaji wa zuri wa upendo wa Baba na Mwana, tunapaswa kuruhusu upendo huo uwatiririkie wengine bila “Kikomo” na bila “Masharti”.

Leo tunaitwa kupenda kwa niaba ya upendo wenyewe, kwa niaba ya Kristo, ambaye ndiye msingi wa upendo wa kweli. Si kwasababu nyingine bali kwa upendo kamili ambao Yesu alitoa kwa ajili yetu. Maisha yetu kama wafuasi wa Yesu yanapaswa kuwa maisha ya kujitoa kwa upendo kwa wengine. Upendo wa Yesu ambao upo ndani yetu unapaswa kutambuliwa, kukukubali na kuupeleka kwa wengine. Hili ndilo lengo la maisha ya Kikristo: kubaki katika upendo wa Kristo na kujazwa furaha. Mimi na wewe tumebarikiwa kufahamu ukweli kwamba MUNGU ni UPENDO. Hivyo tutangaze ukweli huu bila wasi wasi na bila kujibakiza. Kama tutamruhusu Mungu atupende kwa upendo mkamilifu, tutaanza kuona mara moja kwamba upendo huu ukitiririka ndani mwetu kama vile mto wa neema na huruma.

Sala: Bwana, ninakupenda wewe na ninatambua napendwa na wewe. Nisaidie mimi niweze kuwa wazi kwa upendo wako. Nisaidie niweze kufanya upendo huo uzame ndani ili uweze kutiririka kutoka moyoni mwangu na kwenda kwa wengine pia. Yesu, nakuamini wewe. Amina

Maoni


Ingia utoe maoni