Jumapili. 12 Mei. 2024

Tafakari

Alhamisi, Machi 30, 2017

Alhamisi, Machi 30, 2017.
Juma la 4 la Kwaresima

Kut 32: 7-14;
Zab 106: 19-23;
Yn 5: 31-47.


SALA ZINATUBADILI, TUNAKUWA VYOMBO VYA HURUMA YA MUNGU!

Leo somo la kwanza linatuletea swali la kushangaza. Mungu amekasirika, akiwa tayari kuwaangamiza Waisraeli kwasababu ya kuabudu miungu mingine. Lakini Musa, anaongea naye kuhusu uamuzi wake. Tunaweza kushangazwa inawezekana je Mungu wa milele asiye badilika abadili mawazo yake. Ni kitu ambacho tunaweza tusielewe. Ambacho tunaweza kusema kwa ujasiri ni kwamba Maandiko yanatupa ujumbe baada ya ujumbe ukielezea nguvu ya sala. Abrahamu aliongea na Mungu ili asiangamize mji mzima, kama kutakuwa na watu wachache wenye haki, je, kuna watu wachache kati yetu wanaoweza kusali kama Abraham kwa Mungu?

Kazi alizozitenda Yesu zilimpa ushuhuda wa utume aliopewa na Baba yake Mbinguni. Ujumbe wake uliongea na watu jinsi Baba alivyo. Ushuhuda wake ulifunua kiini cha muunganiko wake na Mapenzi ya Baba. Ingawaje miujiza yake ilikuwa ya hali ya juu kwa wote waliokuwa tayari kumwamini, kazi alioifanya ya “pekee” ilikuwa juu ya unyenyekevu na upendo wa kweli. Yesu alikuwa mwaminifu, mnyofu wa moyo kabisa. Kwahiyo, ushuhuda wa matendo yake ya kawaida ya upendo, kujali, na kufundisha ndiyo yalio ziteka na kupata mioyo ya watu wengi. Hata tendo dogo la Upendo liliongea mengi katika mioyo ya watu.

Tutafakari leo, kama tupo tayari kufuata mfano wa Musa na kuwa na muda wa kumfahamu Mungu na kuwa karibu kwa jinsi anavyo tupenda sisi. Je tupo tayari kufungua mioyo yetu kwake ili tuweze kupata huruma yake? Je, tupo tayari kwenda nje kwa wengine ambao hawana bahati kama sisi, ili tuweze kugusa mioyo yao kwa moyo wa Kimungu, kwa kuangalia mahitaji yao? Tutafakari pia wito wetu wakutoa ushuhuda wa Baba yetu wa Mbinguni, kushirikisha upendo wa Baba kwa kila tunaye kutana naye. Kama tutakumbatia utume huu, Injili itafunuliwa kwa wengine kupitia sisi, na mapenzi ya Mungu yatafunuliwa na kutimia katika ulimwengu wetu.

Sala: Bwana, ninaomba niweze kuwa shahidi wa upendo wako utokao moyoni mwako. Nipe neema niweze kuwa mkweli na mwaminifu. Nisaidie mimi niweze kuwa chombo cha uhakika cha huruma ya moyo wako ili kazi zangu zote zishuhudie huruma yako. Yesu, nakumini wewe. Amina.

Maoni


Ingia utoe maoni