Alhamisi. 16 Mei. 2024

Tafakari

Jumatano, Julai 27, 2016

Jumatano, 27 Julai, 2016,
Juma la 17 la Mwaka

Yer 15: 10, 16-21;
Zab 59: 1-4, 9-10, 16-18;
Mt 13: 44-46

JIKANE MWENYEWE ILI UJAZWE!

Fundisho kuu la dini ni sala, hii ni njia ya kuungana na Mungu. Katekisimu ya Kanisa Katoliki inatufundisha kuwa “ Sala ni kuinua moyo kwa Mungu na mambo mema kwa Mungu”. Kawaida tunajikita zaidi katika vitu badala ya Mungu. Inuko ili labadilisha umakini wetu wote, tamanio na upendo kwa Mungu na sio kitu kingine. Ufalme wa Mungu sio sehemu ni Mungu mwenyewe; ni mbingu na milele; ni muunganiko na Mungu. Ni kushiriki katika mafumbo ya Pasaka ya Yesu. Na “kama hali hii ni kuwa kamilifu, tunapaswa kuachana na majadiliano ya kifikra na kurudi katika kiini cha nafsi zetu kwa Mungu kubadilika kabisa kwake yeye” (Mt. Bonaventura). Hili ndilo tualikwalo kulitenda, kila siku, tumia muda fulani katika utupu wa fikra zote na uelewa, na kujitoa wenyewe kwa Bwana. Kama Bwana ni hazina yako pekee, lulu ya kweli, hivyo jikane mwenyewe katika kila kitu.

Sala: Bwana kuwa hazina pekee ya moyo wangu. Amina.

Maoni


Ingia utoe maoni