Ijumaa. 18 Oktoba. 2024

Tafakari

Jumatano, Mei 29, 2024

Jumatano, Mei, 29, 2024
Tafakari ya kila siku
Juma la 8 la Mwaka wa Kanisa

1Pet 1: 18-25;
Zab 147: 12-15, 19-20;
Mk 10:32-45

NJIA AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUSHIKILIA!


“Walikuwa njiani wakielekea Yerusalemu.” Yesu ndiye njia, na njia yake inamleta Yerusalemu, kubeba msalaba wake, kwakukubali kuachia maisha yake kwa upendo wa Baba nakutupenda sisi, akituongoza kwenye ushindi wa mwisho. Wote wanaopenda kuwa wafuasi wake wanapaswa wawe tayari kutembea katika njia hiyo pamoja naye. Wafuasi bado hawajafikia hali hii ya ufuasi. Wakati Yesu akisonga mbele kiaminifu kuelekea Yerusalemu, wafuasi wake wanaonekana kubaki nyuma kidogo. Walikuwa katika hali ya kutoelewa na wote walio wafuata walikuwa katika hali ya woga. Kwajinsi walivyofikiri wao walidhani Yesu hayupo katika mawazo yao. Kwenda Yerusalemu kipindi hiki, ilikuwa nikujitakia matatizo, tena makubwa. Yerusalemu palikuwa ni Sehemu ya mwisho kabisa kwenda.

Yesu kwa upole kabisa anawapa somo jingine, kuhusu nini maana halisi ya kuwa mkubwa katika hali ya ufalme wake. Katika dunia kuwa “mkubwa” ni kuwa na nguvu juu ya wengine, kutawala, kuwa na uwezo wakuwafanya watu wakubaliane na kile unachopenda, kuwatumia watu ili ufikie lengo lako. Lakini katika ulimwengu wa Yesu, ukubwa nikujiweka chini kwaajili ya kuwahudumia wengine, ndugu zetu, majirani, na zaidi sana wale waliowahitaji. Na watu wote kuwatumikia bila kuharibu utu wao. Mamlaka sio kuamrisha, bali kujitoa. Baada ya miaka zaidi ya 2000 ya Ukristo bado ni jambo kubwa sana kwetu kujifunza hili “Mwana wa mtu hakuja kutumikiwa bali kutumikia”.

Sala;
Bwana, badilisha mioyo yetu ya ubinafsi iwe mioyo ya kuwahudumia wengine.
Amina.

Maoni


Ingia utoe maoni