Ijumaa. 03 Mei. 2024

Tafakari

Jumanne, Aprili 16, 2024

Jumanne, Aprili 16, 2024
Juma la 3 la Pasaka

Mdo 7:51-8:1;
Zab 31:3-4,6-8,17,21 (K. 6);
Yn 6:30-35.


YESU ANATOSHA KABISA

Leo, Yesu anatumia njaa na kiu kutufundisha kwamba tunapaswa kuwa na njaa na kiu ya kiroho. Kuna njia moja tu ya kutuliza na kumaliza kiu hii… ni kwa njia yake tu.

Mara nyingi tunapatwa na njaa na kiu. Tunakula na kunywa, lakini baada ya masaa kadhaa tunahisi tena njaa na kiu. Huu mzunguko hatuwezi kuukwepa. Miili yetu daima inadai chakula na kinywaji. Hii ni sawa pia katika maisha ya kiroho. Hatuwezi kusali mara moja na kusema basi inatosha na kumaliza kiu ya kiroho milele. Hatuwezi tu kusema namwamini Yesu mara moja na kubaki tu. Hii ni kwasababu sala na muunganiko na Yesu ni kitu ambacho kinapaswa kuchukua nafasi kila siku.

Ekaristi, “mkate wa uzima” unaridhisha kiu yetu na njaa yetu. Ekarisi ni zawadi ambayo tunapaswa kuitamani na kuipokea daima. Ukweli kwamba tunapaswa kuhudhuria misa na kupokea Ekaristi kila wakati ni ukweli kwamba maisha yetu ya Kikristo yanapaswa kufanywa mapya kila siku.

Kumpenda Yesu na kumfuata yeye ni uamuzi ambao haupaswi tu kufanywa upaya kila siku, bali kufanywa upya kila wakati. Unapaswa kufanywa upya kama unavyo sikia njaa ya kimwili na kiu. Yesu ni mkate wa uzima wa Kiroho na kinywaji cha kweli cha kiroho. Yeye yupo kwa ajili yako. Muache yeye akamilishe hamu ya maisha.

Sala:
Bwana, ninakutamani wewe. Natamani umalize kiu yangu. Nisaidie nikugeukie wewe katika kila kitu. Nisaidie daima nitambue kuwa wewe ni yule ambaye namuhitaji na unatosha. Yesu, nakuamini wewe.
Amina

Maoni


Ingia utoe maoni