Jumapili. 05 Mei. 2024

Tafakari

Jumanne, Januari 23, 2024

Januari 23, 2018
JUMA LA 3 LA MWAKA

2 Sam 6:12-15.17-19
Zab 24:7-10
Mk 3: 31-35


FAMILIA YA MUNGU!


Yesu aliongea mambo mengi yanayo stusha katika utume wake. Katika Injili ya leo kuna aina Fulani ya ukimya unatawala katika umati wa watu wakati Yesu alivyo ongelea kuhusu familia yake. Wengi waliomsikiliza kidogo walidhani Yesu alimkosea heshima Mama yake na ndugu zake. Lakini je ni kweli? Je, unadhani Mama yake alilichukulia hivi? Kwa hakika sio hivyo.

Hili linaonesha kwamba Mama yake zaidi ya wote, ndiye aliye yashika maneno ya Mungu zaidi kuliko wote, na kwamba Mama yake alimtii Mungu na kufanya mapenzi ya Mungu katika ukamilifu wote. Ndugu zake walikuwa muhimu. Lakini Mama yake alikuwa zaidi, kwasababu alitimiza yote kwa utii mkamilifu katika kutii mapenzi ya Mungu. Kwahiyo, kwa utii mkamilifu kwa Mungu, Maria alikuwa mama mkamilifu wa Mwana wa Mungu.

Mara nyingine ujumbe wa Yesu hawakuuelewa. Kwanini hivi? Kwasababu Yesu alijua ni kwa jinsi ghani ya kuwasilisha ujumbe wake na upokelewe vizuri. Alijua ujumbe wake unaweza tu kupokelewa na wale wote waliofungua mioyo yao na kwa Imani. Na alitambua wote walio fungua mioyo yao kwa Imani wataelewa au kutafakari juu ya ujumbe wake mpaka utakapo ingia ndani kabisa. Ujumbe wa Yesu hauwezi kuchukuliwa nakufanyiwa midahalo kama vile ni somo la falsafa. Maria alisikiliza maneno hayo ya Yesu kwa Imani kamili alielewa na alijazwa na furaha. Ilikuwa ni kwasababu ya “NDIO” yake kamili kwa Mungu iliyo mwezesha kuelewa yote aliosema Yesu. Na pia hili lilimsaidia Maria kustahili jina takatifu “Mama” zaidi ya kuwa na uhusiano wa damu. Uhusiano wake wa damu hauna mashaka na nimuhimu, lakini la muhimu zaidi ni muunganiko wake wa kiroho ni muhimu zaidi.

Sisi wote tunaitwa tujiunge kwa undani katika familia hii ya Yesu. Tunaitwa kwenye familia yake kwa njia ya utii wetu wa kutii mapenzi ya Mungu. Tunaitwa tuwe wasikivu, kusikiliza, kuelewa na kutenda yote anayotuambia Yesu. Tuseme “Ndio” kwa Bwana wetu leo, na kuruhusu “Ndio” hiyo iwe ndio msingi wa kujiunga na familia hii ya Mungu.

Sala:
Bwana, nisaidie mimi daima niweze kukusikiliza kwa moyo uliofunguka. Nisaidie niweze kutafakari juu ya maneno yako kwa Imani. Kwa tendo hili la Imani, nisaidie mimi niweze kukuwa katika muunganiko nawe na kuingia katika familia yako ya Kimungu. Yesu nakuamini wewe.
Amina

Maoni


Ingia utoe maoni