Ijumaa. 10 Mei. 2024

Tafakari

Jumamosi, Februari 18, 2017

Jumamosi, Februari 18, 2017,
Juma la 6 la Mwaka

Jumamosi, kumbukumbu ya Bikira Maria

Ebr 11: 1-7;
Zab 145: 2-11;
Mk 9: 2-13.


SHERIA YA DHAHABU YA WAFUASI!

Somo la Injili la leo linatuelezea kuhusu habari ya utukufu wa tukio la kungara kwa sura. Petro, Yakobo na Yohane walienda juu mlimani na Yesu na mara Yesu akageuka sura mbele yao. Alikuwa katika vazi jeupe sana na alikuwa akiongea na Musa na Elia. Mitume walio shuhudia tukio hili walishikwa na hofu kuu na Petro akasema tujenge vibanda vitatu kimoja cha Yesu, kingine cha Musa na kingine cha Elia.Yesu hakujibu kitu kuhusu hili, kwasababu alitambua Petro alitaharuki na hakuweza kufikiria sawa. Musa na Elia ni wazi kwamba hawakuhitaji vibanda.

Moja ya somo la kiroho tunalopata kutokana na somo hili, ni kwamba, wakati tukiwa na nguvu kubwa na kuhisi uwepo wa Mungu katika maisha yetu tunaweza kushawishika kuzidi kipimo na kwenda juu kabisa ambapo tunaweza kuiita ni “kujenga kibanda” . Petro alifurahi sana kiasi kwamba alitaka kubaki pale mlimani. Ni wazi hili lisinge wezekana katika hali ya kufikirika. Si kwamba ni kitu cha ajabu sana yeye kuwa na mtazamo wa namna ile, ni vizuri kutambua na kujifunza kutoka katika hili. Wakati mwingine twaweza kujikuta tukijisikia tukiwa karibu sana na Mungu kwasababu ya kuguswa na wengine au jambo fulani. Wakati hili linatokea, twaweza kujikuta tunapata hisia kubwa sana na kushindwa kufikiria vizuri na kuharibu. Si kushindwa kufikiria juu ya upendo wetu na Mungu, bali tunajikuta tuna furaha iliojikita katika nguvu ya hisia zetu tu, kuliko kujikita kwenye mapenzi ya Mungu. Kutimiza mapenzi ya Mungu, hii ndio maana halisi ya kusema ndio na kuwa na ‘hali ya juu ya kiroho”. Ni kweli tunapaswa kufanya jitihada zaidi ya kuwa na muunganiko wa ndani na Bwana wetu, lakini tunapaswa kutambua kila wakati kwamba hata hisia nzuri hazipaswi kutuongoza kwenye barabara ya mapenzi yetu wenyewe kuliko mapenzi ya Mungu. Mfano, Mungu aweza kukutendea mema, kwasababu ya furaha unasema ngoja leo nikajipongeze kwa (kunywa) na kulewa na kuishia kuharibu!

Maisha ya fadhila ni kuweza kuwa na kiasi. Ingawaje tunapaswa kwa asilimia mia moja kujikabidhi kwa Mungu na mapenzi yake, tunapaswa tutambue kuwa hatupaswi kujivuta katika njia yetu wenyewe au kwa mtu mwingine. Tuombe ili Mungu atuweke katika njia inayo mwelekea yeye daima na kuyafanya mapenzi yake matakatifu.

Sala: Bwana, ninatamani daima kuwa wako kabisa kwa kila njia. Ninatamani kukupenda na kukutumikia kwa utashi, moyo, roho na nguvu. Nisaidie daima nifuate mapenzi yako na yawe mapenzi yako pekee. Ninaomba nisikatishwe tamaa katika njia ulioweka mbele yangu. Ninaomba niishi katika kiasi ili niweze kuishi maisha ya fadhila. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Maoni


Ingia utoe maoni