Jumapili. 19 Mei. 2024

Tafakari

Jumatatu, Januari 15, 2024

Januari 15, 2024

JUMATATU, JUMA LA 2 LA MWAKA

Somo la 1, 1Sam. 15:16-23- Samweli anamwambia Sauli kwamba Mungu amemkataa (Sauli) kuendelea kuwa Mfalme kwasababu amekataa kutii sauti ya Mungu.

Wimbo wa katikati Zab. 50:8-9, 16-17, 21, 23 (K) 23 Nitamwonesha wokovu wa Mungu.

Mk 2: 18-22. Viriba vipya na divai mpya-mila na desturi za zamani zisitufunge tushindwa kupokea na kuishi Injili ya Yesu.


MAISHA YASIO UNGWA, MAISHA MAPYA

Yesu anasema kwamba, hakuna anaye weka divai mpya katika viriba vya zamani, kwani vitapasuka. Kwa hiyo, divai Mpya inawekwa kwenye viriba vipya. Hili linaeleza kwetu kwamba kama tunataka kupokea ujumbe wa Yesu upya na ujumbe wa Injili unao badili maisha, tunapaswa kuwa watu wapya. Maisha yetu ya zamani ya dhambi hayawezi kuchanganywa na zawadi ya neema. Kwahiyo, kama tunataka kupokea ujumbe wa Yesu, ni lazima kuunda maisha mapya sasa.

Yesu anawaonya wafuasi wake kuhusu “akili zilizo fungwa”, zinazo kataa kujifunza kitu kipya. Yesu anatumia picha ambayo imezoeleka kwa wanao msikiliza-viriba vipya na vya zamani. Kama ilivyo na muda maalumu wa kufunga na muda wa kufanya sherehe, vile vile kuna muda wa zamani na muda mpya. Bwana wetu hataki sisi tufungwe na mambo ya zamani tushindwe kuona na kukaribisha maisha mapya ya Roho Mtakatifu katika maisha yetu. Anataka akili zetu na mioyo yetu viwe kama viriba vipya-vilivyo funguliwa na kuwa tayari kupokea divai mpya inayowekwa ndani yetu. Tambua kuwa anataka kuweka neema tele katika maisha yetu kama tutakubali wenyewe kufanywa upya.

Sala:
Bwana, natamani kuwa mpya. Natamani kuisha maisha mapya ya neema ili neema tele ziweze kujazwa ndani mwangu zaidi kwa neno lako. Nisaidie Bwana mpendwa, kukumbatia maisha mapya ya neema ulioweka ndani yangu. Yesu nakuamini wewe.
Amina

Maoni


Ingia utoe maoni