Jumanne. 23 Aprili. 2024

Tafakari

Ijumaa, Aprili 21, 2023

jumaa, Aprili 21, 2023
Juma la 2 la Pasaka

Mdo 5:34-42
Zab 27: 1,4,13-14
Yn 6:1-15


KUFAULU KATIKA JARIBIO LA IMANI!


Mungu daima anatambua anachopenda kufanya. Daima yeye ana mpango mkamilifu wa maisha yetu. Leo katika Injili, Yesu anafanya muujiza wa kuwalisha watu kwa mkate na samaki. Yesu alitambua kwamba ataongeza mkate na samaki ili kuwalisha watu zaidi ya elfu tano. Lakini kabla ya kufanya hili, anamjaribu Philipo. Hivyo hivyo Yesu anatujaribu wakati mwingine. Je, hafanyi hivyo?

Majaribio haya sio kwamba Yesu anapenda kutuuliza tu au kufanya mchezo Fulani na sisi. Bali, anatupa nafasi ya kudhihirisha imani yetu kwake. Jaribio lililopo kwenye Injili lilikuwa ni kumfanya Philipo atumie Imani zaidi kuliko kufikiri kwa kawaida pekee. Philipo aliitwa ili kudhihirisha imani kwamba Mwana wa Mungu yupo pamoja nao pale. Lakini alishindwa jaribio. Alinyoosha mkono kwa ile hali ya kutokuwezekana. Lakini katika hali nyingine ni kama Andrea alikuja kuokoa. Anasema kuna kijana hapa ana mkate na visamaki vichache. Lakini yeye pia alikuwa na Imani kidogo, aliongeza kusema “lakini vya faa nini kwa umati huu mkubwa namna hii?”.

Chembe hii dogo ya imani ya Andrea, ilitosha kwa Yesu kuamuru watu waketi makundi makundi na hivyo kufanya ule muujiza. Inaonekana kwamba Andrea alikuwa na ufahamu kidogo kwamba ilikuwa muhimu kutaja visamaki hivi na mkate. Yesu anavichukua kutoka katika mikono ya Andrea na kuwajali watu.

Mara nyingi tunajikuta katika hali ngumu na hatujui tufanye nini. Tunapaswa kujitahidi kuwa na imani kidogo ili Yesu aweze kuwa na kitu cha kutenda katika maisha yetu. Tunaweza tusiwe na ufahamu wa nini anaenda kufanya, lakini ni lazima kuwa na ufahamu hata kidogo kwamba Mungu ndiye anaye tuongoza sisi. Kama tutaweza hata kukuza Imani hii kidogo sisi pia tutashinda majaribio.

Sala:
Bwana, nisaidie niweze kuwa na Imani kamili ya mpango wako ambao unapenda kuufanya katika maisha yangu. Nisaidie niweze kufahamu kwamba wewe unaongoza na kuyalinda maisha yangu hata pale ninapo ona maisha yanayumba. Katika hali hizo, ninaomba Imani ninayo onesha iwe zawadi kwako ili uweze kuitumia kwa utukufu wako. Yesu, nakuamini wewe.
Amina

Maoni


Ingia utoe maoni