Alhamisi. 28 Machi. 2024

Tafakari

Jumapili, Aprili 16, 2023

Jumapili, April 16, 2023
Dominika ya Pasaka (Dominika ya 2 ya Pasaka)

Acts 5: 12-16;
Ps 118: 2-4, 13-15;
Ufu: 1:9-19
Jn 20: 19-31


HURUMA YA MUNGU ISIYO NA KIKOMO!


"Hakuna mtu atakayetengwa na huruma ya Mungu; kila mtu anajua njia ya kuipata huruma hiyo na Kanisa ni nyumba inayowakaribisha wote na hakuna anayekataliwa. Milango yake inabakia wazi, ili wote wanaoguswa na huruma waweze kupata toshelezo la msamaha. Dhambi inavyokuwa kubwa, vivyo hivyo upendo unapaswa Kuwa mkubwa ule ambao unatolewa na Kanisa kwa wale wote wanaoongoka... Kwa sababu hii, nimeamua kuitisha Jubilei ya hali ya pekee ambayo ni kuwa na huruma ya Mungu katika kiini chake. Unapaswa uwe mwaka mtakatifu wa Huruma. Twahitaji kuuishi mwaka huu katika mwanga wa maneno ya Bwana: "Kuwa na huruma, kama tu Baba yako alivyo na huruma. (Rej. Lk 6:36)." Haya yalikuwa ni maneno ya Papa Francis alipoutangaza mwaka 2016 kuwa ni "Mwaka Mtakatifu wa Huruma."

Leo katika Dominika ya Huruma ya Mungu, tunakumbushwa juu ya huruma ya Mungu isiyo na kikomo. Injili Leo inaonyesha mamlaka ya Yesu pale anapowapa mitume, Roho Mtakatifu, ambaye atakayetoa msamaha wa dhambi.

"Mungu hachoki kamwe kutusamehe; sisi ndiyo tunaochoka kuitafuta huruma yake. Yesu Kristo, aliyetuagiza tusameheane "saba mara sabini" (Mt 18:22) ametupa mfano wake yeye mwenyewe: ametusamehe saba mara sabini... kwa upole usiyotuacha tuaibike, lakini daima wenye uwezo wa kuturudishia furaha yetu, anatuwezesha kuinua vichwa vyetu na kuanza upya. Basi sisi tusiukimbie ufufuko wa Yesu, kamwe tusikate tamaa, hata litokee jambo gani. Maisha yake yawe mfano unaoangazia zaidi ya kitu chochote, unaotusukuma kwenda mbele!" (Furaha ya Injili, 3)

Sala:
Bwana, Nisaidie kamwe nisiwe mbali nawe, badala yake niiamini huruma yako.
Amina.

Maoni


Ingia utoe maoni