Jumapili. 05 Mei. 2024

Tafakari

Alhamisi, Disemba 22, 2016

Alhamisi, Desemba 22, 2016,
Juma la 4 la Majilio

1 Sam 1: 24-28;
1 Sam 2: 1, 4-8;
Lk 1: 46-56


MSIFU MUNGU KILA WAKATI!

Wimbo wa Maria unapaswa kulinganishwa na ule wa Hanna (1 Sam 2: 1-10) na Zakaria (Lk 1: 68-79). Wimbo huu unafunua furaha ya moyo wa Mama wa Mungu. Anakiri mambo makuu aliomtendea Mungu na anaelezea furaha yake ya ndani. Ni vizuri kuona kwamba “moyo” wake na “roho” yake vinafuraha. Vinaelezea matendo yake na matendo ya Mungu. Moyo wa Mama yetu mbarikiwa vinaelezea uwezo wake wa kibinadamu katika akili yake, hisia na matamanio. Hivi ndivyo vinamfanya binadamu. Na katika hali hiyo ya kibinadamu anatangaza ukuu wa Mungu. Kwa maneno mengine, kwa akili yake aliweza kuhisi ukuu wa Mungu, na hivyo anachagua kuutukuza na kuutangaza ukuu wa Mungu na anafanya hivyo kwa hisia zake zote. Utu wake wote ulimezwa na ukuu wa Mungu.

Wakati unabii wa Maria ukisimama katika hali mbalimbali, utofauti wake mkubwa ni katika maana zake. Hanna anamsifu Mungu kwa kumtoa Samueli. Alikuwa katika aibu ya kuwa mgumba (1 Sam 1: 7). Kuzaliwa kwa Samueli kumebadilisha yote hayo, na ana sababu ya kumsifu Mungu. Kadhalika, Zakaria amevumilia kwa muda wa miaka mingi bila kuwa na mtoto na kuwa bubu kwa miezi tisa (Lk 1: 20, 62). Na sasa mtoto wake amezaliwa, na ulimi wake ukafunguliwa, (Lk 1: 64), na ana kila sababu ya kumsifu Mungu. Kwa kulinganisha, tunaona Luka anaweka, sifa za Maria mwanzoni kabisa mwa mimba yake. Alikuwa anamsifu Mungu sio baada tu ya mateso lakini kabla na wakati wa mateso. Alikuwa akisifu katika hali zote. Alikuwa akisifu kwa Imani na sio kwasababu ameona jambo fulani (2 Cor 5: 7).

Je, mimi na wewe tunaiga huu mfano kamili wa Mama yetu mbarikiwa, kama alivyo tafuta kufahamu, kupenda na kutangaza ukuu wa Mungu kwa mwili wake wote? Je, unaruhusu roho Mtakatifu kufurisha moyo wako na furaha? Tuombee kwa ajili ya neema ya Mungu “tutangaze” na “tufurahi” pamoja naye anapozaliwa Mwana wa Mungu, ili wewe pia uweze kuimba wimbo wa furaha!

Sala: Mama mpendwa, ulionesha mfano kamili wa jinsi ya kuishi kwa Imani na uaminifu na unyenyekevu wa mtumishi wa Mungu aliye juu. Ulitangaza ukuu wake na ulijazwa na furaha ya kuja kwake. Nisaidie mimi, kwa maombezi yako yenye nguvu, niweze kuiga Imani yako, kumpenda Mungu kwa moyo wangu wote. Mama Maria niombee mimi. Yesu nakutumainia wewe. Amina

Maoni


Ingia utoe maoni