Jumapili. 05 Mei. 2024

Tafakari

Jumatatu, Disemba 19, 2016

Jumatatu, Desemba 2016,
Juma la 4 la Majilio

Amu 13: 2-7, 24-25
Zab 70: 3-6, 16-17
Lk 1: 5-25


NITAKUWAJE NA HAKIKA?

Inavutia kulinganisha mazungumzo kati ya Zakaria na Malaika Gabriel na yale ya Maria na Malaika Gabriel. Majibu yao kwa malaika Gabrieli yanaonekana kuwa sawa, lakini Malaika Gabrieli anaonekana kumjibu kila mtu kitofauti kabisa. Kwa Maria, malika Gabrieli anaelezea maelezo machache, baada ya ombi la Maria la kutaka maelezo: “Hili linawezekanaje” Maria alisema. Gabriel anajibu “Roho Mtakatifu atakufunika …..” lakini katika hali hii kwa Zakaria hakutoa maelezo. Na badala yake Zakaria anakuwa bubu kwasababu ya kushindwa kuamini. Ingawaje majibu ya Maria na Zakaria yanaweza kuonekana kama yanafanana kwa kuangalia tu katika hali ya kawaida, ni Dhahiri kwamba mioyo yao ilikuwa tofauti. Kwa Maria Mama Mbarikiwa, swali lake aliliuliza katika Imani kamilifu. Alisikia Gabrieli akiongea akaamini. Lakini Imani huwa inatafuta kuelewa, na ndivyo kwa Maria katika Imani timilifu, alitafuta kuelewa fumbo ambalo linakuja kwake. Malaika Gabrieli anajibu kwa kumweleza kwa kifupi, na Maria anafurahi kwa hilo..

Zakaria alimjibu Malaika, “nitajuaje hili?” kwa maneno mengine, anakiri kutoelewa kama maneno haya yatakuwa kweli. Hivyo alikuwa bubu, alama ya kwamba, kama huna Imani, hakuna chakusema.

Kila wakati Mungu anapojifunua kwetu, tunapaswa kwanza kuamini, na kwa unyenyekevu mkubwa, tutafute ufafanuzi. Tufikirie juu ya Imani yetu. Je, tupo tayari kutaka kuelewa na kukubali yote anayotaka kutufunulia Mungu? Je, tupo tayari kukubali na kuamini anayo ongeo Mungu juu yetu? Ingawaje mimi na wewe pengine hatupokei tena neno lake moja kwa moja kupitia kwa malaika kwa kumuona kwa macho, tuna bahati ya kuwa na Mungu akiongea nasi kwa njia ya Neno lake. Je, tunasikiliza na kujibu kwa Imani kama Mama yetu Maria au Zakaria.

Sala: Bwana, ninaomba unipe moyo na Imani kama ya Mama Bikira maria Mtakatifu. Japo, nakubali juu ya udhaifu wangu na dhambi zangu, ninaomba kwa mfano wake na maombezi yake, nipokee kila siku neno lako linalo hubiriwa kwetu. Ninaomba kila wakati niwe makini kwa neno lako na kulipokea kwa moyo wa ukarimu. Yesu nakuamini wewe. Amina

Maoni


Ingia utoe maoni