Jumapili. 05 Mei. 2024

Tafakari

Jumamosi, Disemba 17, 2016

Jumamosi, Desemba 17, 2016,
Juma la 3 la Majilio

Mwa 49: 2, 8-10;
Zab 71: 1-4, 7-8, 17;
Mt 1: 1-17


JE, UNATAMBUA MPANGO WA MUNGU JUU YAKO?

Leo, tunaingia kwenye ‘oktava’ ya kujiandaa kwa karibu kabisa kwa ujio wa Kristo. Kwa siku hii, tunasikia historia ya ukoo wa Yesu. Matayo anatueleza katika mtiririko wa hali tatu ya vizazi kumi na nne. Anaanza na Abrahamu na kumalizia na Yesu. Injii inaanza kwa kumwita Yesu kuwa ni Mwana wa Daudi, Mwana wa Abraham. Hii inaonyesha muunganiko kutoka tangu ahadi za Mungu kwa Abraham, mpaka utimilifu wake katika nafsi ya Bwana wetu Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.

Katika kutimiza ahadi hii, tunaona kwamba Mungu ni mwaminifu. Inachukua karne na karne, ili ahadi yake kwa Abraham itimie, lakini kwa hakika ilitimia. Hili linatueleza wazi kwamba muda wa Mungu na mpango wake juu yetu anajua muda wake wakutimiza ahadi zake, tofauti na jinsi tunavyoweza kufikiri. Tunaweza kuja na mawazo mazuri tukidhani kwamba yatapita. Lakini mara yasipopita mara moja kwa jinsi tunavyodhani na kutumaini, tunaanza kukata tamaa.

Tutafakari juu ya mipango alionayo Mungu juu ya maisha yetu. Inaweza isiwe kama tunavyodhani na kutabiri au kadiri ya jinsi tunavyoomba katika sala. Lakini inaridhisha kwamba ni kwa ajili ya uzuri wetu, ni kwasababu ya muunganiko wetu naye Mbinguni. Yesu alizaliwa ili atuvute karibu zaidi nae. Leo Yesu anatutaka mimi na wewe tuweke mipango yetu kwake na mitazamo yetu kwake. Anahitaji haya na mengine mengi. Anataka tujikabidhi sisi wenyewe kwenye mpango wake mkamilifu ndani ya moyo wa Baba yetu wa Mbinguni.

Sala: Bwana, natambua kwamba njia zako ni kamilifu na kwamba mipango yako ni mikamilifu sio yangu. Nisaidie niachane na tamaa zangu na nijikabidhi zaidi kwako, na kukuamini kabisa, na kwa yote uliopanga kwa ajili yangu. Bwana, hekima yako ni kamilifu. Nisaidie niweze kuamini hilo kwa moyo wangu wote. Yesu nakuamini wewe. Amina

Maoni


Ingia utoe maoni