Jumapili. 08 Septemba. 2024

Tafakari

Jumatano, Novemba 09, 2016

Jumatano, Novemba 9, 2016,
Juma la 32 la mwaka wa Kanisa

Sikukuu ya Kutabarukiwa kwa Basilika la Laterani

Ez 47:1-2, 8-9, 12;
Zab 45:2-3, 5-6, 8-9;
1Kor 3: 9-11, 16-17;
Yn 2:13-22


HEKALU LA MUNGU!

Katika mwaka 592 Kabla ya kuja Kristo, Eziekeli alikutana na Mungu aliyemtumia kama chombo, kwanza kuwaandaa watu wadhambi kwa maangamizi na baadae kutabiri juu ya utengenezwaji upya wa hekalu. Baada ya muda mfupi 535 BC, ukaanza ujenzi wa hekalu chini ya Zerubabeli aliyerudi kutoka utumwani Babeli na wayahudi zaidi ya 42,000. Ujenzi ulikamilika 518 BC..

Hili hekalu la pili lilijengwa katika hali ya kifahari chini ya Herodi mkuu ambaye alitaka kumua Yesu, kama familia takatifu isingekimbilia Misri. Hili ni hekalu ambalo Wayahudi walifanya sehemu ya kuuzia vitu na Yesu akawafukuza. Alitawanya fedha zao na kupindua meza, akiwatoa ngombe na kondoo njee na alisema “…achene kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa sehemu nyumba ya biashara”. Maneno haya ya Yesu mara nyingi yaliwakasirisha viongozi. Lakini zaidi, jibu la Yesu juu ya wao kutaka ishara ili kutoa ushuhuda wa anayo yafanya ulikuwa juu ya uwezo wao wa kufikiri. Yesu alikuwa akiongelea kuhusu hekalu ambalo lilikuwa mwili wake mwenyewe, ambao haujajengwa na mawe, lakini wao walikuwa wakiongelea kuhusu hekalu lilojengwaa na Herodi.

Kwa hili hekalu jipya la Agano jipya, Mt. Paulo anasema leo katika somo la pili “hamkujua kwamba miili yenu ni hekalu la Mungu ambapo Roho wa Mungu anaishi ndani yenu?” Mwili wa Kristo (Kanisa) lilizaliwa baada ya mwili wa Yesu kufa pale kalvari na pazia la hekalu kupasuka kutoka juu mpaka chini (Mt 27: 50-51).

Yesu anatuambia leo, sisi pia ni mahekalu ya Roho Mtakatifu, wa Mungu. Tukiwa tumeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu, sisi ni mahekalu yalio barikiwa. Kama viumbe wanao jitambua tunaweza na tunaalikwa kuitikia uwepo wa Mungu ndani mwetu, kuwa hekalu binafsi na katika hali ya pekee. Leo tukiwa tunasherekea kutabarukiwa kwa basilika la Laterani, mama wa makanisa yote ya Kikatoliki ulimwenguni pote, tujenge tena upya hali ya umoja na mshikamano ambazo zitatujenga na kututambulisha kila wakati kama wajumbe wa mwili wa Kristo.

Sala: Bwana Yesu, kama ulivyo takasa hekalu, nitakase nami pia, nioshe, nifanye mpya, nifanye nistahili kukupokea. Amina

Maoni


Ingia utoe maoni