Jumapili. 08 Septemba. 2024

Tafakari

Jumanne, Novemba 08, 2016

Jumanne, Novemba 8, 2016,
Juma la 32 la Mwaka wa Kanisa

Tit 2:1-8, 11-14;
Zab 36:3-4, 18, 23, 27, 29;
Lk 17:7-10

MTUMISHI MWAMINIFU!

Katika somo la kwanza tunamuona Paulo akiendelea kumwambia Tito, aendelee kunena maneno ya uzima yenye kuwaelekeza watu wa rika mbali mbali katika maisha ya ufuasi wa Kristo. Na zaidi sana wanadamu wote wanaongozwa na neema ya Mungu ili waweze kupingana na yote duniani yasio endana na mapenzi ya Mungu. Wazee, wa kike na wakiume na vijana wawe watu wakiasi, wazima katika Imani, upendo na saburi, wazee wawe mfano kwa watoto wao. Hizi ni sifa za mtumishi mwaminifu wa Kristo anayetambua kuwa yeye ni mtumishi tu, na kwamba kila afanyalo linapaswa kuwa kwaajili ya sifa na utukufu wa Mungu.

Katika hali hiyo hiyo, somo la Injili leo Yesu anatutaka tutambue ya kuwa sisi ni watumishi tu tulioko duniani. Kila tulicho nacho,pamoja na maisha yetu ni zawadi ya bure kutoka kwa Mungu na kama viumbe vyake sisi ni mali yake. Nguvu zetu, muda na vyote tulivyo navyo ni mali ya Mungu ni kwa ajili ya sifa na utukufu wake. Kama Yesu alivyokuja, “si kutumikiwa bali kutumikia” tunapaswa kuwa watumishi wanyenyekevu wa Mungu, tukimtumikia Mungu na jirani zetu kwa uhuru kamili. Kila zawadi tutakayo pokea itakuwa ni neema na sio kama kutafuta faida, na hatimaye mwisho wa nyakati kwa watumishi wa aminifu, Bwana atawaambia “vyema mtumishi mwema na mwaminifu”(Mt 25:21)

SALA: Bwana, nisaidiye nibaki mnyenyekevu ili niweze kukutumikia wewe na jirani zangu bila kutaka faida. Amina

Maoni


Ingia utoe maoni