Alhamisi. 19 Septemba. 2024

Tafakari

Jumatatu, Juni 20, 2016

Jumatatu, Juni, 20, 2016,


Juma la 12 la mwaka wa Kanisa




2 Fal 17: 5-8, 13-15, 18;


Zab 59: 3-5, 12-13;


Mt 7: 1-5




USIHUKUMU!


Katika Injili ya leo Yesu anatuambia tusiwahukumu wengine. Kwanini tusiwahukumu wengine? Kwanza kabisa, washiriki wa ufalme wa Mungu wanapaswa kuachia hukumu kwa hakimu wa mwisho (Mungu). Kama Bwana wao wanapaswa wajiingize katika kuponya nakuyafanya yote upya. Kurekebishana kindugu sio kuhukumu, lakini pia namna ya kurekebisha inapaswa kuwa na roho nzuri. Msukumo daima uwe kumpenda jirani yangu kama nafsi yangu.

Pili, hatuwezi kujua nafsi ya mtu asilimia mia moja. Ni vigumu na huenda haiwezekani kwa mwanadamu kuwa mwema kabisa katika kuhukumu mtu. Hakuna mwanadamu aliye mkamilifu kabisa anayeweza kumuhumu mwanadamu mwingine. Ni bora kuangalia makosa yetu wenyewe na kuachia mapungufu ya wengine kwa Mungu. Tusitangaze dhambi za wengine kwani sio kazi yetu, tutambue na sisi pia tungeweza kuanguka au kokosea kama wao. Tuwasaidie wenzetu pale wanapo anguka ili warudi tena kwa Baba yetu wote mwenye huruma. Sisi wote ni wakosefu tunahitaji neema ya Mungu. Kuna usemi unaosema “Tunacho ona kwa wengine ni kidogo sana kulinganisha na kile tusicho kiona”. Tuishi kindugu tukichukuliana katika madhaifu yetu, na tunapokosea tujue hakuna cha zaida zaidi ya kutubu na kumrudia Mungu. Kunyoosheana kidole sio kazi yetu. Mungu angehesabu maovu yetu hakuna mwanadamu angeweza kujidai au kutamba kuwa mwema. Tusihukumu turekebishane kindugu na kwa upendo, tukishikana mikono wote tupelekana Mbinguni kwa Mungu Baba yetu wote.



Sala:

Bwana mwenye huruma, nisaidie mimi niweze kutengeneza mwenendo wangu kwanza, kabla ya mimi kujitoa kuwarekebisha wengine.


Amina.

Maoni


Ingia utoe maoni