Kanuni ya Imani
Nasadiki kwa Mungu, Baba Mwenyezi, mwumba mbingu na dunia.
Na kwa Yesu Kristu, Mwanaye wa pekee, Bwana wetu; aliyetungwa kwa Roho Mtakatifu,
akazaliwa na Bikira Maria,
akateswa kwa mamlaka ya Ponsyo Pilato,
akasulubiwa, akafa, akazikwa, akashukia kuzimu;
siku ya tatu akafufuka katika wafu;
akapaa mbinguni; amekaa kuume kwa Mungu Baba Mwenyezi;
toka huko atakuja kuwahukumu walio hai na wafu.
Nasadiki kwa Roho Mtakatifu,
Kanisa takatifu katoliki,
ushirika wa Watakatifu,
maondoleo ya dhambi,
ufufuko wa miili, uzima wa milele.
Amina.
0 Imependwa
0 Maoni
Maoni
Ingia utoe maoni