Sala ya Asubuhi
Ee Baba yetu Mungu Mkuu,
Umenilinda usiku huu,
Ninakushukuru kwa moyo,
Ee Baba, Mwana na Roho,
Nilinde tena siku hii,
Niache dhambi nikutii,
Naomba sana Baba wee,
Baraka yako nipokee,
Bikira safi ee Maria,
Nisipotee unisimamie,
Mlinzi Mkuu Malaika wee,
Kwa Mungu wetu niombee,
Nitake nitende mema tu,
Na mwisho nije kwake juu.
0 Imependwa
0 Maoni
Maoni
Ingia utoe maoni