Jumapili. 05 Mei. 2024

Sala

Kanuni ya Imani ya NICEA

Nasadiki kwa Mungu Baba Mwenyezi
Mwumba mbingu na nchi na vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana.
Nasadiki kwa Bwana mmoja Yesu Kristu,mwana wa pekee wa Mungu.
Aliyezaliwa kwa Baba tangu milele yote.
Mungu aliyetoka kwa Mungu,mwanga kwa mwanga,Mungu kweli kwa Mungu kweli.
Aliyezaliwa bila kuumbwa, mwenye umungu mmoja na Baba,
ambaye vitu vyote vimeumbwa naye.
Ameshuka toka mbinguni kwa ajili yetu sisi wanadamu na kwa ajili ya wokovu wetu.
Akapata mwili kwa uwezo wa roho mtakatifu kwake yeye Bikira Maria akawa mwanadamu.
Akasulibiwa pia kwa ajili yetu sisi
Akateswa kwa mamlaka ya Ponsyo Pilato,akafa akazikwa.
Akafufuka siku ya tatu ilivyoandikwa.
Akapaa mbiguni, amekaa kuume kwa baba
Atakuja tena kwa utukufu kuwahukumu wazima na wafu nao ufalme wake hautakuwa na mwisho
Nasadiki kwa Roho Mtakatifu Bwana mleta uzima atokaye kwa Baba na Mwana anayeabudiwa na kutukuzwa
pamoja na Baba na Mwana aliyenena kwa vinywa vya manabii.
Nasadiki kwa Kanisa moja,Takatifu Katoliki la mitume
Naungama ubatizo mmoja kwa maondoleo ya dhambi.
Nangojea na ufufuko wa wafu.
Na uzima wa milele ijayo.

Amina.

Maoni

Loberei Araule

Nahitaji PDF ya hii kanuni

Ingia utoe maoni