Sala ya Usiku
Sasa siku imekwisha,
Kwako Mungu napandisha,
moyo wangu kwa shukrani,
nipumzike kwa amani,
Mema mengi umenipa,
ninashindwa kukulipa,
Baba mwema ondolea,
yote niliyokosea.
Yesu mpenzi unijie,
ombi langu usikie,
unifiche mtoto wako,
ndani ya jeraha zako,
Ewe Mama unipe neema,
raha na usiku mwema,
Roho mlizi ukakeshe,
pepo wasinikoseshe
Naiweka roho yangu,
mikononi mwa Baba yangu,
bila hofu napumzika,
mwisho kwake nitafika.
Amina
1 Imependwa
4 Maoni
Maoni
Elia Stanley Mlay
Ee Mungu naomba usiku huu ninapoenda kulala ukanikinge na pepo wachafu,majinamizi,wachawi,vibwengo ,nilale salama pamoja na watoto wangu sita AMENAndrew Timotheo
Ee MUNGU mwingi wa rehema na baraka uturinde usiku huu mimi na familia yangu utupe usingizi mnono mikononi mwako vichwa vyetu twajilaza wewe uu mkuu leo hata milele AminaJoseph Marekani
Ee mungu nibaliki tunapo enda kulala maraika mlinzi awe pamoja nasi na tuamke na fulaha na upendo aminaMarekani Nestory
Mungu wangu wabaliki watu ote wanao fuatilia mkatoliki leo walale salama na waamke wenyenguvu na afya tele aminaIngia utoe maoni